NGODAZ

moto moto news
HOTUBA YA MGOMBEA URAIS
KUPITIA CHAMA CHA CHADEMA
NA UKAWA MH. EDWARD
NGOYAI LOWASSA YA KUZINDUA
ILANI NA KAMPENI YA
UCHAGUZI MKUU
Jangwani-Dar-es-Salaam, 29 AGOSTI 2015
Ndugu Wana Dar es salaam na Watanzania
wenzangu
Leo ni siku ya kihistoria. Baada ya miaka ishirini
na tano tangu mfumo wa vyama vingi
urejeshwe, vyama vya upinzani wa CHADEMA,
CUF, NCCR na NLD umeungana chini ya Umoja
wa Katiba ya Wananchi kupigania uchaguzi
mkuu wa mwaka huu na kuwa na mgombea
mmoja katika ngazi zote.
Miaka zaidi ya hamsini ya utawala wa serikali
za CCM na waasisi wake, umekuwa utawala wa
wachache walio hodhi madaraka na mali za
nchi.
Leo tunaanza safari ya uhakika ya kuleta
mabadiliko ya kweli nchini.
Mabadiliko yaletayo neema na kujenga upya
mfumo wa uchumi, haki na sheria nchini.
Mabadiliko ya kuimarisha huduma za jamii kama
elimu, afya, maji na makazi.
Mabadiliko ya kuondoa umaskini.
Mabadiliko tunayatoahidi ni mabadiliko ya
kurejesha matumaini kwa Watanzania kwa
kubadili hali zao za maisha.
Kila mwaka hali na ubora wa maisha ya
Watanzania imeshuka wakati tunaambiwa kuwa
pato laTaifa linakuwa.
Lakini Watanzania wanachotaka siyo takwimu
bali kuona kipato chao kinakua, shule, hospitali
na barabara bora zinajengwa.
Wanataka kupata maji safi na salama ya
kunywa. Wanataka makazi bora.
CHADEMA na UKAWA, tuna dhamira ya kuleta
mabadiliko ya kweli ili kuona azma ya
Watanzania tangu uhuru ya kuondoa umaskini,
maradhi,na ujinga inahitimishwa.
Ili tufanye hivyo tuahitaji tufanye mabadiliko ya
fikra, uongozi, sera na utendaji.
Leo Tanzania inakabiliwa na changamoto nyingi
za ki-uchumi, kisiasa na kijamii. Changamoto
hizi ni matokeo ya sera za utawala wa Chama
kimoja wa miaka hamsini. Sote ni wahanga wa
siasa na sera hizi.
Miaka Hamsini ya CCM imetosha. Tunataka
mabadiliko na siyo ahadi zile zile kila mwaka
Tusidanganyike, CCM hawana jipya
Chagueni UKAWA wenye dira ya kubadili maisha
ya wananchi.
Mimi ninauchukia umaskini na mimesimamia
maendeleo kwa vitendo. Nilipokuwa Waziri Mkuu
nilijaribu kubadili hali hii. Nilisimamia ujenzi wa
shule za kata, Chuo Kikuu cha Dodoma.
Nilihakikisha mikataba mibovu ya maji inavunjwa
na sasa wananchi wa kanda ya ziwa wanapata
maji safi.
Ndugu watanzania
CCM wanauliza tuna mpango gani wa kumaliza
umaskini. Sisi hatuahidi tu. Tutatenda.
Ilani yetu ni dira ya kuondoa umaskini kwa
mikakati sahihi na siyo nadharia.
Mkakati wa kuondoa umaskini si wa sekta kwa
sekta bali wa sekta zote kwa pamoja. Ni ujumla
wa utendaji na utekelezaji wa sera za kila sekta
utakao leta maendeleo.
Mkakati wangu na UKAWA wa kuondoa umaskini
utakuwa na nguzo tano:-
Kupunguza matumizi ya serikali na mashirika
yake na kuimarisha utendaji na uwajibikaji.
Kukuza pato la serikali kwa kudhibiti ukwepaji na
misamaha ya kodi holela na kuhakikisha nchi
inawekeza katika sekta muhimu na inapata
gawio halisia kutoka wawekezaji
Kukuza uchumi kwa sera na sheria endelevu
ikiwa ni pamoja na kukuza biashara na
uwekezaji hasa katika sekta za madini, kilimo,
viwanda, ufugaji na uvuvi na kuondoa kodi kwa
wanyonge.
Kuimarisha huduma za umma kama elimu, afya,
maji na makazi, na mazingira
Kuimarisha utawala bora na mfumo wa haki na
sheria chini ya Katiba ya Wananchi.
Chini ya misingi hii na ili kufanikisha mkakati wa
kuondoa umaskini, serikali yangu itafanya
yafuatayo:-
ELIMU BORA KWA KILA MTANZANIA
Nimelisema hili huko nyuma. Nalisema tena leo.
Elimu kwanza, Elimu kwanza, Elimu kwanza.
Kwa hiyo mkakati wetu wa msingi utakuwa
kutoa Elimu itatayogharamiwa na serikali kwa
kila Mtanzania kutoka elimu ya msingi hadi Chuo
Kikuu na pia:-
Kuimarisha elimu ya teknolojia, ustadi na ufundi
inayojenga uwezo wa kujiajiri na ushindani
katika soko la ajira.
Ujenzi na uimarishaji wa miundombinu ya elimu
ikiwa ni pamoja na shule za Kata.
Kusimamia ubora wa viwango vya elimu kote
nchini.
Kuimarisha taaluma na mitaala katika mashule.
Kuondoa utoro darasani, na kuboresha afya za
wanafunzi.
Kuboresha maslahi na vitendea kazi kwa walimu
ikiwa ni pamoja na nyumba, posho ya
kufundishia, usafi

HOTUBA YA MGOMBEA URAIS KUPITIA CHAMA CHA CHADEMA NA UKAWA MH. EDWARD NGOYAI LOWASSA YA KUZINDUA ILANI NA KAMPENI YA UCHAGUZI MKUU Jangwani-Dar-es-Salaam, 29 AGOSTI 2015 Ndugu Wana Dar es salaam na Watanzania wenzangu Leo ni siku ya kihistoria. Baada ya miaka ishirini na tano tangu mfumo wa vyama vingi urejeshwe, vyama vya upinzani wa CHADEMA, CUF, NCCR na NLD umeungana chini ya Umoja wa Katiba ya Wananchi kupigania uchaguzi mkuu wa mwaka huu na kuwa na mgombea mmoja katika ngazi zote. Miaka zaidi ya hamsini ya utawala wa serikali za CCM na waasisi wake, umekuwa utawala wa wachache walio hodhi madaraka na mali za nchi. Leo tunaanza safari ya uhakika ya kuleta mabadiliko ya kweli nchini. Mabadiliko yaletayo neema na kujenga upya mfumo wa uchumi, haki na sheria nchini. Mabadiliko ya kuimarisha huduma za jamii kama elimu, afya, maji na makazi. Mabadiliko ya kuondoa umaskini. Mabadiliko tunayatoahidi ni mabadiliko ya kurejesha matumaini kwa Watanzania kwa kubadili hali zao za maisha. Kila mwaka hali na ubora wa maisha ya Watanzania imeshuka wakati tunaambiwa kuwa pato laTaifa linakuwa. Lakini Watanzania wanachotaka siyo takwimu bali kuona kipato chao kinakua, shule, hospitali na barabara bora zinajengwa. Wanataka kupata maji safi na salama ya kunywa. Wanataka makazi bora. CHADEMA na UKAWA, tuna dhamira ya kuleta mabadiliko ya kweli ili kuona azma ya Watanzania tangu uhuru ya kuondoa umaskini, maradhi,na ujinga inahitimishwa. Ili tufanye hivyo tuahitaji tufanye mabadiliko ya fikra, uongozi, sera na utendaji. Leo Tanzania inakabiliwa na changamoto nyingi za ki-uchumi, kisiasa na kijamii. Changamoto hizi ni matokeo ya sera za utawala wa Chama kimoja wa miaka hamsini. Sote ni wahanga wa siasa na sera hizi. Miaka Hamsini ya CCM imetosha. Tunataka mabadiliko na siyo ahadi zile zile kila mwaka Tusidanganyike, CCM hawana jipya Chagueni UKAWA wenye dira ya kubadili maisha ya wananchi. Mimi ninauchukia umaskini na mimesimamia maendeleo kwa vitendo. Nilipokuwa Waziri Mkuu nilijaribu kubadili hali hii. Nilisimamia ujenzi wa shule za kata, Chuo Kikuu cha Dodoma. Nilihakikisha mikataba mibovu ya maji inavunjwa na sasa wananchi wa kanda ya ziwa wanapata maji safi. Ndugu watanzania CCM wanauliza tuna mpango gani wa kumaliza umaskini. Sisi hatuahidi tu. Tutatenda. Ilani yetu ni dira ya kuondoa umaskini kwa mikakati sahihi na siyo nadharia. Mkakati wa kuondoa umaskini si wa sekta kwa sekta bali wa sekta zote kwa pamoja. Ni ujumla wa utendaji na utekelezaji wa sera za kila sekta utakao leta maendeleo. Mkakati wangu na UKAWA wa kuondoa umaskini utakuwa na nguzo tano:- Kupunguza matumizi ya serikali na mashirika yake na kuimarisha utendaji na uwajibikaji. Kukuza pato la serikali kwa kudhibiti ukwepaji na misamaha ya kodi holela na kuhakikisha nchi inawekeza katika sekta muhimu na inapata gawio halisia kutoka wawekezaji Kukuza uchumi kwa sera na sheria endelevu ikiwa ni pamoja na kukuza biashara na uwekezaji hasa katika sekta za madini, kilimo, viwanda, ufugaji na uvuvi na kuondoa kodi kwa wanyonge. Kuimarisha huduma za umma kama elimu, afya, maji na makazi, na mazingira Kuimarisha utawala bora na mfumo wa haki na sheria chini ya Katiba ya Wananchi. Chini ya misingi hii na ili kufanikisha mkakati wa kuondoa umaskini, serikali yangu itafanya yafuatayo:- ELIMU BORA KWA KILA MTANZANIA Nimelisema hili huko nyuma. Nalisema tena leo. Elimu kwanza, Elimu kwanza, Elimu kwanza. Kwa hiyo mkakati wetu wa msingi utakuwa kutoa Elimu itatayogharamiwa na serikali kwa kila Mtanzania kutoka elimu ya msingi hadi Chuo Kikuu na pia:- Kuimarisha elimu ya teknolojia, ustadi na ufundi inayojenga uwezo wa kujiajiri na ushindani katika soko la ajira. Ujenzi na uimarishaji wa miundombinu ya elimu ikiwa ni pamoja na shule za Kata. Kusimamia ubora wa viwango vya elimu kote nchini. Kuimarisha taaluma na mitaala katika mashule. Kuondoa utoro darasani, na kuboresha afya za wanafunzi. Kuboresha maslahi na vitendea kazi kwa walimu ikiwa ni pamoja na nyumba, posho ya kufundishia, usafi

Read More