
Kundi la wanamgambo wa kikristo
nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati la anti-Balaka limewaachilia huru
watoto 163 waliokuwa wakitumikishwa na kundi hilo ikiwa ni sehemu ya
utekelezaji wa ahadi liliyotoa kupitia mpango wa amani unaosimamiwa na
Umoja wa Mataifa. Watoto hao ni miongoni mwa watoto zaidi ya 6,000
wanaoaminika kuwa wamekuwa wakitumikishwa kufanya kazi duni zikiwemo za
upishi na usafishaji au kutumiwa kama wapiganaji na makundi yanayobeba
silaha nchini humo. Mohamed Malick Fall, afisa wa Mfuko wa Watoto wa
Umoja wa Mataifa UNICEF lililosimamia zoezi la kuachiliwa huru watoto
hao katika mji wa Batangafo huko kaskazini mwa Jamhuri ya Afrika ya
Kati, amesema hatua hiyo ni ishara ya utekelezaji wa ahadi zilizotolewa
na viongozi wa makundi ya wanamgambo ikiwa ni sehemu ya mchakato wa
amani na maridhiano. Ameongeza kuwa mamia ya watoto wengine wanatarajiwa
kuachiliwa huru kabla ya kumalizika mwaka huu. Zaidi ya watoto 350
waliachiliwa huru na makundi yanayobeba silaha mnamo mwezi Mei.
Kwengineko katika koloni hilo la zamani la Ufaransa mapigano mapya
yamezuka katika mkoa wa kati wa Bambari na kusababisha watu wapatao 10
kuuawa baada ya wanamgambo wa kikristo wa anti- Balaka kumuua kwa
kumkata kichwa kijana wa Kiislamu mwenye umri wa miaka 19…/
(chanzo tehran radio)
0 maoni:
Chapisha Maoni