Aliibuka mfungaji mabao bora katika ligi ya klabu bingwa Afrika na kusaidia klabu hiyo kutwaa ubingwa mwaka jana.
Samatta alibwaga Baghdad Boundjah (Algeria/ Etoile du Sahel) na Robert Kidiaba (DR Congo/ TP Mazembe) kutwaa tuzo hiyo.
Sherehe ya kutangaza washindi wa tuzo hizo zilifanyika mjini Abuja Nigeria usiku. Ingawa habari zilitokea usiku, baadhi ya magazeti yalihakikisha yamechapisha habari za ushindi wake.Samatta baadaye aliweka kwenye Twitter picha hii inayomuonyesha akiwa na tuzo yake na akiwa amejifunika kwa shiti yenye rangi za bendera ya Tanzania.
0 maoni:
Chapisha Maoni