NGODAZ

moto moto news

Mwanamke Muislamu afurushwa mkutano wa Trump


Baraza la uhusiano mwema la kiislamu nchini Marekani limemtaka mgombea wa urais kwa tiketi ya chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump, kuomba msamaha kwa kuamrisha mwanamke wa dini ya kislamu kufurushwa kutoka kwa mkutano wake wa kisiasa.
Rose Hamid alilalamikia wito wa bwana Trump wa kuweka marufuku ya muda kwa waislamu wanoingia nchini Marekani.
Umati uliyokuwemo ulifanya kelele za kejeli na maafisa wa usalama wakamwondoa.
Bi Hamid mwenye umri wa miaka 56 na ambaye anafanya kazi ya huduma katika kampuni ya moja ya ndege ,baadaye aliamrishwa na afisa mmoja wa usalama kuondoka.
Alizomwa wakati alipokuwa akifurushwa katika mkutano huo.
Wafuasi wa Trump walipoketi, mwanamke huyo alisimama kwa ukimya, huku akivalia vazi lililokuwa na maandishi, salaam. Nimekuja kwa amani.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

Chapisha Maoni