Kiungo wa kati wa Chelsea Oscar
amekanusha habari kwamba alihusika kwenye mfarakano na mchezaji mwenzake
Diego Costa wakati wa mazoezi.
Gazeti la Telegraph liliripoti
kwamba ilibidi wachezaji hao wawili kutenganishwa baada yao kushikana
mashati Costa alipomchezea visivyo Oscar.Lakini Oscar, mwenye umri wa miaka 24, ameandika kwenye Twitter kwamba hawezi akapigana na mchezaji mwenzake, na kumweleza mshambuliaji huyo wa Uhispania, mwenye umri wamiaka 27, kama “mmoja wa marafiki wangu wakubwa”.
Chelsea watakutana na klabu ya ligi ya daraja la tatu Scunthorpe katika raundi ya tatu ya Kombe la FA Jumapili.
0 maoni:
Chapisha Maoni