
Zaidi ya viongozi wakuu mia moja wa
kanisa la Kianglikana wametia saini barua ya kulitaka kanisa la
Uingereza kutubu kwa kuwabagua wakristo wanaoshiriki mapenzi ya jinsia
moja, watu wanaoshiriki mapenzi na jinsia zote mbili na wale walio na
jinsia mbili.
Barua hiyo inayoelekezwa kwa askofu mkuu wa
Canterbury na York, inasema kuwa wakristo hao wamekuwa wakichukuliwa
kama raia wa daraja la pili.
Mkutano wa viongozi wa makanisa yote ya kianglikana unaanza hapo kesho nchini Uingereza.
Mkutano
huo unatarajiwa kutawaliwa na gumzo kuhusu jinsia huku wanachama wa
kanisa hilo ambao wanapinga mapenzi ya jinsia moja sasa wanawataka
Waanglikana kutubu kwa kuwatukuza viongozi wa kanisa hilo ambao ni
wapenzi wa jinsia moja.
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
0 maoni:
Chapisha Maoni